8/10/2004

Dar Es Salaam, Julai 2003:

Nimeingia kwenye ofisi ya serikali. Binti anayepokea wageni ameketi anaongea na mtu kwenye simu yake ya mkono. Inaelekea wanaongea mambo yanayohusu harusi. Mambo ninayoyasikia ni kama,
“Ehe, hizo kadi ndio zinatolewa lini?”
“Na kikao kinafanyika lini na lini?
“Sare tunashona nini?”
"Lakini ndugu yako yule naye, yaani pale ndio amefika? Yaani mabinti wote wazuri pale ofisini kwake ameshindwa kupata wa kuoa?"

Nimesimama namtazama. Nimekuja ofisi hii ya serikali ninahitaji huduma. Hii ni ofisi ya serikali yangu. Ananyanyua macho na kunielekeza kwa kichwa niketi kwenye viti vikuukuu vilivyopo pembeni. Ninaketi. Kiti kinatoa mlio kama vile kinataka kuvunjika. Ninashtuka. "Kaa tu usiogope." Ananiniambia na kuendelea na gumzo. Mara anatokea binti mwingine akiwa na rundo la magazeti ya udaku. Anayaweka mezani, "Ukimaliza kusoma mpatie Halima. Bosi wake kaenda Bagamoyo kwenye semina. Kaboreka kweli. Hana kazi." Ananitazama kisha anamuuliza mwenziye, “Umemhudumia huyu kaka?”
“Bado,” anamjibu.
“Maliza basi simu hiyo umhudumie, mimi hadithi yangu ile ya wiki iliyopita nataka kuimalizia kabla Shomari hajaja. Nimemuomba anipeleke Kariakoo mara moja.”

Shomari ni dereva wa moja ya magari ya ofisi hii ya umma. Magari haya wanayatumia kama yao binafsi!

“Kaka samahani, hivi hizo ni nywele zako?," anayetaka kumalizia hadithi ya gazetini ananiuliza huku akitafuta ukurasa wenye hadithi yenyewe. Maneno yanashindwa kunitoka kwa kutokuamini ninachoshuhudia mbele ya macho yangu.

Ofisi ya umma imefanywa kama sebuleni kwa mtu! Sijaulizwa kilichonileta hapa. Sijahudumiwa. Naulizwa juu ua nywele zangu!

Naitazama ofisi hii. Nawatazama mabinti hawa wawili waliojichubua. Ninatikisa kichwa. Watanzania tunaamka asubuhi na mapema, sio kujenga nchi bali kuibomoa!

1 Maoni Yako:

At 8/10/2004 03:18:00 AM, Anonymous Anonymous said...

GULP ....

TAKE OFF UR TOP...

NOW THE REST....

SAY...... GULP *BREATHES DEEPLY*

SAY .....

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com