8/18/2004

Hadithi: Mtoto wa Kizungu na mtoto wa Kichagga!

"Mbona huwa unanikodolea macho sana?" Nimeamua kuvulia maji nguo. Kila siku ninasema nitamuuliza. Leo nimeamua.
"Nakukodolea macho?" Ananiuliza huku akipitisha mkono kichwani kurudisha nywele zake ndefu nyuma.
"Ndio. Hakuna ubaya. Ninapenda kujua kwanini."

Ananitazama. Anatabasamu. Ananitazama tena. Kama ilivyo mazoea yake, anapitisha kichwani vidole vyake vyembamba vyenye kucha zenye matunzo kurudisha nywele nyuma. Yaelekea anapenda nywele zake sana. Jina lake ni Lisa. Mama ni mtaliano. Baba Mmarekani.

"Unataka nikwambie kwanini nakutazama?" Ananiuliza.
"Nataka uniambie ndio maana nimekuuliza."
"Napenda nywele zako." Anasema huku anatoa tabasamu la aibu. Kisha anarudisha nywele nyuma. Safari hii hatumii vidole. Anatikisa kichwa kidogo upande mmoja. Nywele zinatii amri.
" Naomba kushika nywele zako"

ITAENDELEA...
*******************************************************************************
Ndugu yangu kisa hiki kitaendelea. Rudi tena hapa ili usipitwe.

2 Maoni Yako:

At 8/18/2004 12:54:00 PM, Anonymous Anonymous said...

Mbona umekatisha uhondo mzee?

 
At 8/24/2004 09:52:00 AM, Blogger Ndesanjo Macha said...

muhimu hadithi iendelee

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com