7/03/2005

Nimetoka kuwasikiliza jamaa wa Yes Men

Toka asubuhi tulikuwa kwenye mkutano mbadala wa G8. Tumewasikiliza jamaa wengi kama Samir Amin, Walden Bello, Trevor Ngwane (toka Afrika Kusini). Toka asubuhi ilikuwa ni kusikiliza, kuandika, kupiga makofi, na mbinja. Pia tumeweza kuhojiana na mama mmoja toka World Development Movement juu ya sakata la ubinafsishaji maji katika jiji la Dar Es Salaam. Mama huyu amekuwa akilifuatilia suala hilo kwa muda.

Lakini yote nadhani tukio kuu kwangu leo ni kukutana na kuwasikiliza jamaa wa Yes men. Jamaa hawa ambao hujifanya kuwa ni wawakilishi wa mashirika makubwa kama WTO, Benki ya Dunia, n.k. hualikwa kwenye mikutano na watu wanaoamini uongo wao ambao kwao ni aina ya harakati. Walituonyesha filamu mbalimbali za matukio ambayo wameshiriki bila kujulikana kuwa wao ni jamaa tu wasio na uhusiano wa mashirika wanayowakilisha. Wamewahi kuhojiwa na BBC, CNBC (ya Marekani) bila vituo hivi vya luninga kujua kuwa walikuwa wanahoji watu ambao sio. Watembelee hapa nyumbani kwao.

1 Maoni Yako:

At 7/06/2005 05:04:00 AM, Anonymous Anonymous said...

Hao yes men walionyeshwa kwenye kipindi cha televisheni jumatatu iliyopita hapa matawi ya chini.
Wamekubuhu masihara!

Tunga

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com