7/07/2005

LEO GLENEAGLES

Leo nimekuwa hapa Gleneagles toka asubuhi, usisahau kuwa chakula ni cha bure!! Nimekuwa nikizunguka huku na kule kutafuta Waafrika toka vyama visivyo vya kiserikali na pia waandishi wa habari toka Afrika. Nimemuona mwandishi mmoja toka Tanzania, Ayoub Mzee, ambaye anafanya kazi Sky Channel hapa Uingereza.

Kuna wanaharakati wachache sana toka vyama visivyo vya kiserikali hapa Gleneagles. Jamaa fulani kaniambia kuwa wengi wako Edinburgh, hawakutaka kuja hapa. Eti wanafurahia maisha ya Uskoto. Hapa nimeona wanaharakati wanne tu. Nimewahoji tayari. Habari hiyo nitaiwekea kiungo hapa ikishatoka. Pia nimehoji baadhi ya waandishi wa habari wa Afrika. Nitamaliza kesho. Kati ya maswali ambayo nimekuwa nikiwauliza wanaharakati ni hili: ukipata nafasi ya kunywa kahawa na akina Joji Kichaka utawaambia nini?

Usiniulize mimi swali hili maana sitakubali kutumia muda wangu kunywa chai na Joji. Chai haitashuka.

Kesho ndio ilikuwa tuondoke kurudi London ambako kama mnavyojua kumetoka janga kubwa. Ila kwasababu viongozi wa Afrika watafaongea na waandishi jioni, imebidi tukae hapa hadi jumamosi. Je nikikapa nafasi ya kumuuliza Mkapa swali nimuulize nini?

2 Maoni Yako:

At 7/07/2005 02:32:00 PM, Blogger Indya Nkya said...

Muulize alichofuata hapo. Baada ya hapo muulize yeye ni kiongozi wa watanzania au wa wahisani?

 
At 7/08/2005 12:25:00 PM, Anonymous Anonymous said...

Muulize what his legacy? after selling out our country.

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com