4/18/2005

MAKALA MPYA MBILI ZA PADRI KARUGENDO

Kuna makala mpya mbili motomoto za Padri Karugendo. Ya kwanza inazumguzia mjadala ulioendeshwa na Tido Mhando wa BBC na Profesa Chachage na Mama Luhane kuhusu Papa Paulo. Kichwa chake ni: Papa Yohane Paulo: Hasi na Chanya. Isome hapa. Nyingine inauliza juu ya ukimya wa upinzani kipindi hiki ambacho moto wa uchaguzi mkuu tayari umewashwa. Isome hapa. Makala zake nyingine ziko kwenye kona yake, Kalamu ya Padri Karugendo chini ya makala zangu na Freddy Macha. Sijapandisha makala zangu muda kidogo. Nitafanya hivyo leo. Pia baadhi mmeniuliza mbona nimekuwa kimya kuhusu kifo cha Papa Paulo. Nadhani nimetaka nyoyo za watu zitulie kwanza kabla sijasema lolote.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com