12/28/2004

SAMAHANINI

Wazalendo wote, wana wa nchi, wazawa, wana mapinduzi, wakereketwa, wafurukutwa, wana ngangari, wana ngunguri, wana apollo (kule Mererani), vijana wa kule kwa mzee Jomo na "baba" Moi (sasa?), marastafari, vizabizabina, bila kumsahau mshikaji Joji Dabliyuu Kichaka, Wana mageuzi na mageuzo, wapiga debe, majangili yanayovaa kofia ya "uongozi," makaburu wanaoitwa "wawekezaji," polisi wanaokamata wahalifu huku nao ni wahalifu, wahubiri wanaotangaza wokovu wakati tunahitaji mapinduzi, mahakimu wanaohukumu wala rushwa huku nao wanakula rushwa (mbele, nyuma, kushoto, na kulia)...bila kuwasahau wana mapanga sha sha sha...! NIMERUDI. Samahanini kwa ukimya.
Bado siamini kuwa wale jamaa wenye ngozi isiyo na kemikali za melanin (Wayoruba wa Nigeria huwaita, "watu waliochubuka") waliomuua dada yetu wameachiwa!
Hiyo baadaye. Ngoja nitafute kitu cha kwanza cha kukupa. Nina mambo yamejaa vyungu kumi na mbili. Nitaanza kupakua chungu namba saba.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com