12/24/2004

DUA LANGU LITASIKILIZWA?

Kuna siku nilisema kuwa ningekuwa na uwezo ningefanya binadamu waweze kuendesha magari wakiwa wamelala! Hii ingenisaidia usiku wa leo wakati nikielekea Vermont, mwendo wa masaa kumi na kitu...kama hakutakuwa na theluji. Kumbe kwa uwezo wa teknolojia huenda ikawezekana siku moja. Tazama hapa.
Kingine nilichosema ni kuwa ningekuwa na uwezo ningefanya binadamu tuweze kusoma tukiwa usingizini! Na pia ningeongeza masaa ya siku, yaani siku iwe na masaa zaidi ya 24.
Usishangae mbona mawazo ya ajabu ajabu namna hii, ukiwa ughaibuni lazima mawazo kama haya yakujie!

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com