12/24/2004

ANGEKUWA NI KABWELA/MZALENDO MWENZETU...

Kawaida sina tabia ya kuapa. Lakini leo naapa. "Hakya" nani vile...nikatike kichwa (Nalamba udongo na kulamba kidole kisha kukielekeza mawinguni tunakoamini ndio aishipo muumba). Angekuwa ni kabwela, mlalanjaa, ngozi nyeusi, mzawa, mzalendo kama wewe na mimi ametuhumiwa kuua angeonja joto ya jiwe lupango hadi amani ipatikane Mashariki ya Kati.
Faili lingepotea.
Tungeambiwa, "ushahidi unaendelea" kwa miaka mitano hata kumi.
"Vizibiti" vingepotea.
Baadhi ya mashahidi wangetoweka.
Wengine wangekufa.
Mara hakimu angefiwa.
Mara angepata dharura.
Mwendesha mashtaka angeumwa. Angepona. Angeumwa. Angepona.
Mwendesha upelelezi angehamishwa kituo.
Mwendesha upelelezi mpya angehitaji nusu mwaka au mwaka mzima kupitia kesi....
Ingekuwa balaa, nuksi, mkosi, bahati mbaya, uzembe, utumbo, ubadhirifu, rushwa, ufisadi ...taja mengine.
Huyo ni mwenzetu.
Lakini wanapokuwa ni wale jamaa tunaowaabudu ambao mungu, yesu, na malaika wanafanana nao, na hata miti ya krisimasi tunaiwekea pamba ili iwe kama hali yao ya hewa ilivyo (hali yao ya hewa ina uungu fulani...!).
Akiwa ni jamaa mwenye damu ya jamaa waliomhadaa Mangungo wa Msovero...
unajua kitakachotokea.
Kama hujui...Hebu tazama.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com