12/29/2004

MSIKILIZE JOE TUNGARAZA

Niliwahi kukutaka utege sikio kusikiliza kipindi cha AFROWORLD kinachoendeshwa na Mtanzania Nambiza Joe Tungaraza (DJ Joe) toka Australia kupitia Radio Adelaide 101.5 kila jumamosi. Masaa niliyoweka wakati ule ni ya Australia, ambapo ni saa 10:30 usiku hadi saa sita usiku. Leo naweka masaa ya sehemu nyingine ili muweze kukifuatilia. Hiki ni kipindi cha matukio na muziki kuhusu Waafrika (Afrika na Ughaibuni). Muziki aina mbalimbali kama Makossa, Zouglou, Rhumba, Kwaito, Rai, Highlife, Reggae, African hiphop unatumbuizwa. Na pia mjadala wa matukio ya kisiasa, kijamii, kitamaduni, na kiuchumi yanayohusu Waafrika.
Unachotakiwa kufanya ni kwenda kwenye tovuti ya Radio Adelaide kila jumamosi: www.radio.adelaide.edu.au na ukishafika hapo kongoli palipoandikwa "Listen Online."

Masaa ndio haya (shukran Tunga):
Walioko Marikani: Midwest/East Coast: Saa 1 asubuhi.
West Coast: Saa 10 alfajiri.
Johannesburg: Saa 8 mchana.
DarEsSalaam: Saa 9 Alasiri.
London: Saa 6 mchana.
Amsterdam: Saa 7 mchana.
Oslo, Stokholm, Copenhagen : Saa 7 mchana.
Helsinki: Saa 8 mchana.





0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com