12/21/2004

BABA AKIFARIKI...

Rafiki yangu, John Hill, kanishtua kweli. Hivi majuzi nilimuuliza, "Hivi unafanya nini mwisho wiki?" Akaniambia kuwa anakwenda kumtembelea baba yake. Akaongeza, "Nikimtembelea huwa tunacheza pool na kutazama mpira kwenye luninga."

Akanyamaza kidogo kisha akasema, "Baba yangu ana hela nyingi sana na ameshazeeka. Najua atafariki wakati wowote. "
Nikashtuka. "Unasema baba yako atafariki?!"
"Ana shinikizo la damu. Amelazwa hospitali mara mbili hivi karibuni. Hana muda mrefu. Baba yake, yaani babu yangu, alikufa kwa shinikizo la damu...akifariki nitarithi hela zake na pikipiki zake mbili. Ana hela nyingi sana benki."
Nilibaki mdomo wazi. Alikuwa anaongea kama vile ni jambo la kawaida. Bado ninaisikia sauti yake kichwani mwangu. Sijammaliza.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com