12/19/2004

MABISHANO YA ALI MAZRUI NA HENRY GATES, JR.

Filamu ya Wonders of the African World ilileta mabishano na mijadala mizito mizito kati ya wanahistoria, wana taaluma, waandishi, n.k. Mabishano makali kati ya Ali Mazrui na Henry Lous Gates (mtengenezaji wa filamu hiyo na mwalimu katika chuo kikuu cha Harvard) yalisambaa kila kona ya mtandao wa tarakilishi (kama yalivyokuwa mabishano kati ya Ali Mazrui na Wole Soyinka ambayo nitayaweka hapa baadaye). Ingawa mabishano haya ya kitaaluma yaliyokea muda mrefu (mwaka 1999), masuala yanayozungumziwa yanahitaji kuwa katika mijadala na fikra za watu wanaotafuta ukweli juu ya historia na utamaduni wa watu weusi.

Chini ya uchambuzi wa Ali Mazrui, kuna uchambuzi wa Molefi Kete Asante, mmoja wa waanzilishi wa dhana AFROCENTRICITY. Pia kuna uchambuzi wa Tolber, Jr. na Martin Doudou. Baadaye nitaweka majibu ya Henry Gates kwa Ali Mazrui. Faidi uhondo wa elimu na maarifa kwa kwenda kwenye mabishano hayo hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com