11/19/2004

KENYA: URAIA UWILI UKO NJIANI

Naona Wakenya huenda wakaruhusiwa kuwa na uraia uwili. Nimepata habari hii toka kwenye blogu nzuri sana ya Ory Okolloh iitwayo Kenyan Pundit. Nadhani suala la uraia uwili kwa Tanzania ni muhimu sana. Watawala wetu wanapenda sana kutuambia kuwa dunia inakuwa kijiji (dunia-kijiji) na kuwa hizi ni zama za utandawazi. Dhana hizi mbili, utandawazi na dunia-kijiji, zinatulazimisha kukubali kuwa uraia uwili ni jambo ambalo halihitaji mabishano marefu. Kinachohitajika ni mjadala wa kisera na kujifunza toka kwa nchi zenye sheria za uhamiaji zinazoruhusu uraia uwili. Watanzania tunaweza vipi kuishi katika dunia-kijiji kama sheria za nchi yetu zinatubana kuweza kufaidi uraia wa dunia? Bonyeza hapa usome habari hiyo kuhusu Kenya.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com