10/14/2004

SIKU YA KUMUENZI NYERERE

Eti leo ni siku ya kumuenzi Mwalimu Nyerere Tanzania! Watu wanapumzika. Kisha? Kisha kesho wanakwenda kazini hadi mwaka ujao tena! Sijui ni watu wangapi wanamuenzi kwa dhati.

Mwezi wa saba mwaka huu niliandika kipande hiki juu ya Nyerere. Kwa heshima yake nitabandika tena ili ambao hawakupata kusoma wasome. Pia kama unataka kusikiliza hotuba zake, mwisho wa nukuu kuna sehemu ya kubonyeza ili umsikilize.

MWALIMU NYERERE AWAPASHA BENKI YA DUNIA
Mwaka 1999 Ikaweba Bunting alifanya mahojiano na Mwalimu Nyerere. Mahojiano hayo yalitolewa katika gazeti la New Internationalist. Nimependa sana jibu lake hili. Hivi ndivyo alivyosema:
"I was in Washington last year. At the World Bank the first question they asked me was `how did you fail?' I responded that we took over a country with 85 per cent of its adult population illiterate. The British ruled us for 43 years. When they left, there were 2 trained engineers and 12 doctors. This is the country we inherited. When I stepped down there was 91-per-cent literacy and nearly every child was in school. We trained thousands of engineers and doctors and teachers. In 1988 Tanzania's per-capita income was $280. Now, in 1998, it is $140. So I asked the World Bank people what went wrong. Because for the last ten years Tanzania has been signing on the dotted line and doing everything the IMF and the World Bank wanted. Enrolment in school has plummeted to 63 per cent and conditions in health and other social services have deteriorated. I asked them again: `what went wrong?' These people just sat there looking at me. Then they asked what could they do? I told them have some humility. Humility - they are so arrogant!"
Ndio Mwalimu huyo. Ukitaka mahojiano kamili kongoli hapa.
Ukitaka kusikiliza hotuba za Mwalimu Nyerere kongoli hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com