10/13/2004

MKAPA, HUU NDIO UZAWA!

Baadhi ya Watanzania walipoanza kuhubiri uzawa, yaani umuhimu wa kuwawezesha Watanzania ili waweze kushiriki kikamilifu katika soko huria, uwekezaji, na ubinafsishaji; walionekana kuwa wanahubiri itikadi ya ubaguzi wa rangi. Idd Simba alipofikia hatua ya kuandika kabisa kitabu juu ya uzawa, chama chake, CCM, kilikuja juu na kusema kuwa hiyo siyo sera rasmi ya chama hicho.

Sasa leo nimepigwa na butwaa baada ya kusoma aliyosema Rais Mkapa (hivi nilitakuwa kusema Mheshimiwa? Sina uhakika, ila sina tabia ya kuita watawala Waheshimiwa. Waheshimiwa kwa lipi?) jana katika mkutano uitwao Annual Global African Business Titans jijini Dar Es Salaam. Aliyosema yote kwa neno moja tunaita UZAWA. Nasubiri CCM wamjie juu mwenyekiti wao. Nimefurahishwa na ujumbe alioutoa Mkapa. Ila ningependa kama angetumia muda huo kutupa ripoti, takwimu, na mifano ya sera na sheria ambazo serikali yake imepitisha kumsaidia huyu mzawa ili aweze kupambana na wafanyabiashara toka nje wenye mitaji mikubwa na uzoefu wa muda mrefu wa biashara ya kimataifa. Badala ya kutuambia kuwa "Tunapaswa kusaidia wazawa..." atuambie amefanya nini toka awepo madarakani kufanikisha analosema? Huu ndio ujumbe tunaoutaka. Soma aliyosema Mkapa kwa kubonyeza hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com