6/08/2005

TAMASHA LA "LIVE 8": WAAFRIKA NI WATAZAMAJI TU?

Bob Geldoff anakumbukwa kwa kampeni ya kuchangisha fedha kwa ajili ya waliokumbwa na baa la njaa Afrika miaka 20 iliyopita. Kampeni hiyo iliitwa Live Aid. Hivi sasa Geldoff, ambaye ni mmoja wa wajumbe wa Tume ya Afrika, anaongoza kampeni nyingine iitwayo Live 8. Katika kampeni hii, kutakuwa na matamasha ya muziki katika miji mbalimbali huku Ughaibuni. Tofauti na Live Aid, kampeni hii haitafuti fedha bali inakusanya sauti za watu wanaoamini na kusema kuwa “sasa imetosha.” Msikilize Mandela akiongea kuhusu mradi wa Live 8.
Katibu mkuu wa Pan African Movement yenye makao yake makuu Kampala, Uganda, Dk. Tajudeen Abdul Raheem, anasema kuwa kampeni hii ni mfano wa harakati mbalimbali duniani za kuwasaidia Waafrika ambazo haziwahusishi Waafrika. Anasema kuwa Live 8 ni sawa na kinyozi anayenyoa nywele huku anayenyolewa akiwa hayuko. Soma uchambuzi wake hapa.


0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com