6/07/2005

KUTOKA MKUTANO WA COMMONS-SENSE: FAIDA ZA KUTOA VITABU BURE MTANDAONI

Hakuna ambaye hakushawishika baada ya kumsikiliza mwanamama Eve Gray ambaye alizungumzia umuhimu wa wachapishaji barani Afrika kuanza kutoa vitabu vyao bure kwa njia ya mtandao wa Intaneti na teknolojia nyingine za kisasa. Mada yake iliyotolewa siku ya kwanza ya mkutano wa Commons-Sense ilitokana na utafiti alioufanya kwa ajili ya jamaa hawa Hapa. Utafiti wake unaonyesha kuwa kuna uwezekano wa wauza vitabu kuongeza mauzo wakitoa vitabu vyao bure mtandaoni. Mwanzoni watu wengi tulijiuliza, "Utaongezaje mauzo kama utakuwa ukitoa vitabu bure? Mauzo hayo yatatokana na kumuuzia nani? Jibu ukitaka soma mada yake kamili hapa. Mwanauchumi wa Pambazuko soma kwa undani uniambie.
Moja ya mambo aliyosema Gray yaliyoshtua washiriki wengi na kuwafanya kuona umuhimu wa teknolojia rahisi za kupeana na kuhifadhi habari na maoni kama blogu ni kuwa mambo yote yaliyoko katika mtandao wa intaneti asilimia 0.4 tu ndio inatoka Afrika. Ukiondoa Afrika Kusini mchango wa Afrika unabaki kuwa ni asilimia 0.02!

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com