12/31/2004

UNAJUA HAYA KUHUSU MWAKA MPYA?

Watu wengi hudhani kuwa mwaka mpya wa kirumi husherehekewa na watu wote duniani. Wafuasi wa imani ya Bahá'í , kwa mfano, wanasherehekea mwaka mpya Machi 21 (siku hiyo huitwa NaW Ruz. Kalenda ya Ki-Bahá'í ina miezi 19 yenye siku 19. Imani ya Bahai ilianzishwa na Bahá'u'lláh. Wachina nao wana mwaka mpya wao. Sijui kama unajua kuwa miezi ya kichina ni majina ya wanyama. Kongoli hapa kwa undani zaidi. Nchini Thailand, mwaka mpya uitwao Songkran husherehekewa Aprili 13 hadi 15 kwa kurusha maji. Mwaka mpya wa Kikeltiki, Samhain, husherehekewa mwezi wa Novemba. Kalenda ya Kirumi ya zamani ilikuwa na miezi 10, na mwaka mpya ulianza Machi Kwanza.

Kalenda inayotumika katika nchi nyingi hivi sasa ni Kalenda ya Kiregori ambayo ilichukua nafasi ya Kalenda ya Juliani. Kanisa Katoliki lilipendelea kubadilisha kalenda ya Juliani kwasababu kadhaa, mojawapo ikiwa ni kufanya waumini wa kikristu washerehekee pasaka karika siku iliyokubaliwa na Baraza la Nikea. Huko Abisinia (Ethiopia) mwaka mpya (enkutatash) ulisherehekewa mwezi wa tisa tarehe 11. Kumbuka kuwa Abisinia iko nyuma miaka saba na miezi nane ya kalenda ya Kiregori (Giriligoloyo kwa wale waliosome Song of Ocol and Lawino) inayotumika katika nchi nyingi duniani hivi sasa. Kalenda ya Ethiopia ina miezi 13. Waislamu nao wana kalenda yao ambayo inafuata majira ya mwezi badala ya jua kama ilivyo kalenda ya kirumi. Kalenda hii ni pungufu kwa siku 11 tofauti na ile inayofuata majira ya jua. Mwaka mpya kwenye Uislamu huwa ni mwezi wa pili. Mwaka 2005 kwenye kalenda ya Kiislamu ni mwaka 1426. Mwaka wa Kiislamu unaanza toka pale mtume Muhammada na wafuasi wake walipokimbilia Medina toka Maka (mwaka 632 katika kalenda ya kirumi).

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com