8/29/2004

HOJI, USIOGOPE

Barua za watu wanaowasiliana nami zinaonyesha kuwa watu wengi bado wanatawaliwa na hofu ambayo imekuwa ikitumiwa na wanasiasa na dini kutupumbaza na kutufanya watumwa. Usiogope kuhoji lolote lile. Wewe kama biandamu una haki ambayo haitoki kwa mtu yeyote (awe rais, hakimu, polisi, kasisi au shehe) ya kuhoji kila kitu. Hoji. Pinga. Iwe ni serikali. Iwe ni dini. Uwe ni mfumo wa elimu. Iwe ni sheria. Iwe ni desturi. Una haki hiyo na hakuna kiumbe ambaye ataweza kukuzuia ukikataa kuwa kondoo.

Watatokea watu watakwambia kuwa ukihoji serikali utafungwa. Anayekwambia hivyo ndiye anapaswa kufungwa. Hoji serikali. Kama serikali uliyoichagua au iliyochaguliwa na wengi (kwa mujibu wa tume yao ya uchaguzi) haiwakilishi matakwa yako, kuna jambo moja la kufanya. IONDOE MADARAKANI. Iangushe. Ipindue. Chukua madaraka. Jiongozeni wenyewe!

Wengine watakwambia kuwa ukihoji mambo ya dini au Mungu utakuwa kichaa. Au utakwenda motoni. Wanaokwambia hivi tayari wanaungua. Muhoji hata Mungu. Anapenda sana kuhojiwa. Utawasikia wakisema, "Tafuteni nanyi mtaona," "Watu wangu wataangamia kwa kukosa maarifa." Laiti wangejua maana ya maneno haya.

Ndugu yangu, hoji usiogope. Kuhoji ni mwanzo wa uhuru.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com