6/13/2004

kesho ni mbio

Ngoja nikalale maana kesho ni jumatatu. Mbio zinaanza. Nchi hii inajengwa kwa mbio. Hakuna muda wa kupoteza. Kesho usiku nitatazama sinema inaitwa Matrix. Nitakueleza kidogo juu ya sinema hii (ina sehemu tatu) nikishaimaliza.

Halafu jumatano ninapanga kwenda kwenye msikiti wa waislamu weusi. Hawa ni tofauti na waislamu ambao unawafahamu hapo Tanzania. Sio Sunni wala Shia. Wakati Sunni na Shia wanaamini kuwa Muhammada alikuwa nabii wa mwisho. Waislamu wa kundi la Nation of Islam wanaamini kuwa hakuwa nabii wa mwisho. Nitakupasha kidogo juu ya ziara yangu msikitini kwao.

Nitakunywa maji ya moto na asali kisha nilale.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com