6/13/2004

jumapili

Nimechelewa kulala jana usiku. Mwili umechoka kweli. Leo jumapili. Siku ya "kujifanya." Kila mtu leo anajinfanya kuwa mcha mungu. Kisha kuanzia jumatatu hadi jumamosi wanakuwa "wacha shetani."

Siku ya jumapili ni siku ninasikia harufu ya unafiki hewani. Ukienda kanisani usisahau kupeleka kodi ya wiki: sadaka.

Nakwenda mjini kwenye msikiti wa Taifa la Waislamu (nation of islam). Yaani waislamu weusi. NInakwenda kutafuta kanda za mahubiri ya Louis Farrakhan. Kisha nirudi nije nikapike, nile na kuketi kutazama mikanda.

Baadaye.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com