6/05/2005

SIKILIZA MAHOJIANO YANGU REDIO UFARANSA

Nimemaliza kufanya mahojiano kwa njia ya simu na Radio France Internationale, idhaa yake ya kiingereza, kuhusu vuguvugu la kujenga blogu za Kiswahili na lugha nyingine za Kiafrika. Mwanamama aliyenihoji, Cordelia Hebblethwaite, kanitumia maelezo ya kuwasaidia wale watakaopenda kusikiliza mahojiano hayo redioni au kwenye mtandao wa kompyuta. Ujumbe wake huo hapo chini. Tafsiri ya Kiswahili ni ya kwangu:
"Nenda hapa. Vipindi vyote viko mkono wa kulia. Mahojiano yatarushwa katika kipindi kimoja kati ya vinne vya asubuhi vinavyokwenda kwa jina la "English to Africa." Saa ni hizi: 04.00 GMT, 05.00 GMT, 06.00 GMT, 07.00 GMT. Vipindi vya jumatatu vitakuwa mtandaoni kwa masaa 24 kisha nafasi yake itachukuliwa na vipindi vya siku ya jumanne. Vipindi vya asubuhi huanza kwa habari, kisha baada ya kama dakika 15 mahojiano mbalimbali huanza kurushwa. Sehemu hiyo ndipo mahojiano yako yatakuwepo."

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com