2/28/2005

MAHOJIANO YANGU NA MREMA WA TLP

MAHOJIANO KATI YANGU NA MWENYEKITI WA CHAMA CHA TANZANIA LABOUR PARTY, AUGUSTINE LYATONGA MREMA:

Ndesanjo: Jina lako nani vile?
Mrema: Agustino Lyatonga Mrema.
Ndesanjo: Agustino? Inaandikwa A-G-U-S-T-I-N-O au inaandikwa A-U-G-U-S-T-I-N-E?
Mrema: Hembu rudia...

Naamua kumwandikia kabisa. Anasoma kisha anasema kuwa jina lake ni Augustine. Nami namwambia mbona haitamkwi Agustino?

Mrema: Tuendelee na masuala ya maana yaliyokuleta hapa ndugu mwandishi.
Ndesanjo: Hili ni moja ya masuala ya maana yaliyonileta hapa. Suala hili linaitwa utumwa wa
akili. Kwanini unakuwa na jina ambalo hata kulitamka huwezi? Unadhani kuwa hili
sio suala la maana?
Mrema: Wewe umetumwa na CCM! Lazima ni shushushu wa CCM.
Ndesanjo: Hapana, nimetumwa na mizimu ya mababu zako. Wanasikitika mno. Wanatoa
machozi kila kukicha na kabla ya kwenda kulala. Wanasema
mambo unayofanya yanasikitisha sana. Kwa mfano, niambie kirefu cha jina la kile
chama ulichohamia baada ya kuondoka CCM (yaani NCCR). Wananiambia kuwa
uliingia chama chenye jina ambalo hata kusema kirefu chake ulikuwa hujui.

** Inaendelea baadaye. Nimekuonjesha utamu kidogo.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com