2/14/2005

HISTORIA YETU: UNALIJUA ZIWA NAMLOLWE?

Ziwa Namlolwe ni ziwa ambalo hivi sasa, kutokana na ukoloni na utumwa wetu wa mawazo waliotuachia wakoloni, linaitwa Ziwa Vikitoria (Lake Victoria.) Waluo walikuwa wakiliita ziwa hili Namlolwe.
Huyu malkia mwenye ziwa Afrika Mashariki sijui alitufanyia nini watu wa Afrika Mashariki kiasi cha kuamua kulipa ziwa hili jina lake. Hivi kuna ziwa au mto gani kule Uingereza uliopewa jina la Mwafrika?
Kule Zimbabwe kuna maporomoko yanaitwa Maporomoko ya Vikitoria (Victoria Falls). Jina la asilia la maporomoko haya ni Mosi O Tunya (yaani moshi utoao mlio kama radi).

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com