1/11/2005

MARTIN LUTHER KING, JR

Tunamkumbuka mhubiri, mtetezi wa haki, na mwanaharakati Dr. Martin Luther King, Jr. Kuna mengi sana ya kujifunza toka kwake. Hasa kwa vijana ambao wanajaribu kuleta mabadiliko nchini Tanzania, Kenya na kwingineko. Kwa kipindi hiki ambacho mahubiri ya jino kwa jino, ngangari na ngunguri yamechukua sura mpya katika siasa nchini Tanzania...kwani sasa kuna kitu kinaitwa "mapanga sha sha sha..."...harakati za watu ambao waliamini kuwa binadamu ana uwezo wa kuleta mabadiliko ya kweli kwa njia za amani zina mengi ya kutufunza. Watu kama Dr. King waliamini kuwa hata kama siri-kali mnayotaka kuibadili ina maguvu ya dola na inatumia maguvu hayo kunyamazisha raia na hata kuua, ziko njia za amani zinazoweza kushinda. Alisema kuwa hapendi dhana ya jicho kwa jicho maana haki inapokuja kupatikana kunakuwa hakuna mwenye macho! Haya, nenda hapa.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com